Featured post

HABARI KATIKA PICHA: ZIARA YA KWANZA YA MBUNGE WA KWANZA WA JIMBO LA ULYANKULU JOHN PETER KADUTU

MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA DINI VIONGOZI WA DINI WAKIFUATILIA HOTUBA YA MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUT...

Sunday, 13 December 2015

IJUE:HISTORIA FUPI YA MTEMI MILAMBO




Mtemi Milambo alizaliwa mwaka 1820 eneo lililojulikana kwa jina la Ikonongo na alipewa jina la Mbula Kasanda. 

Baba yake mzazi na Mtemi Milambo aliitwa Kasanda na mama yake alijulikana kwa jina la Mwasi Mpela.

Babu yake na Mtemi Milambo aliyejulikana kwa jina la Kasele Muhofu na ambaye aliishi miaka 300 baada ya kuzaliwa mwaka 1520 na kufariki mwaka 1820 alimrithisha utemi mjukuu wake Mbula Kasanda (Milambo).

Babu yake Mtemi Milambo, Kasela Muhofu kwa maajabu aliongea akiwa tumboni mwa mama yake kabla ya kuzaliwa na baada ya kuzaliwa hakunyonya maziwa ya mama yake.

Mbula Kasanda (Mtemi Milambo) kabla ya kutawazwa kuwa mtemi alitanguliwa na watemi tisa wa kwanza akiwa Sibuga aliyetawala kuanzia mwaka wa 22BK akafuatiwa na Mkindo wa Kwanza ambaye alirithiwa na Mlowa na kisha kufuatiwa na Moto wa Tatu.

Moto wa Tatu alirithiwa na Nsimba Nchembe ambaye naye alimwachia utawala Kapaya aliyerithiwa na Kasele Muhofu ambaye alimuachia utawala Kasimana Kasele.

Kasimana Kasele alikabidhi utawala kwa Mkindo wa Pili ambaye alimrithisha Mbula Kasanda maarufu kama “Mtemi Milambo.”

Mtemi Milambo alianza kutawala mwaka 1838 katika eneo la Ikonongo huku akiwa na Ikulu mbili za Ikonongo na Iselamagazi.

Kabla ya kifo chake kilichotokana na homa kali, Mtemi Milambo aliacha urithi wa kiti cha utemi kwa mtoto wake wa kike aliyejulikana kwa jina la Kibete mnamo mwaka wa 1884.

Kibete alizaliwa akiwa na ziwa moja yaani titi moja la mkono wa kushoto.

Kabla ya Kibete kufariki alikabidhi kiti cha utemi kwa Solomoni Kazwika Milambo ambaye alizaliwa siku ya Jumatatu asubuhi ya tarehe 18 Julai, 1945 ambaye yupo hadi hivi sasa.

Solomoni Kazwika Milambo kabla ya kuzaliwa aliongea akiwa tumboni mwa mama yake na hakunyonya maziwa ya mama yake.

 

KADUTU: “NITASIMAMIA UBORESHAJI WA MAKUMBUSHO YA MTEMI MILAMBO”




Na Paul Christian, Ulyankulu.

Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani Tabora Mheshimiwa John Peter Kadutu ameahidi kuboresha mazingira ya makumbusho ya Mtemi Milambo yaliyopo katika eneo la Ikonongo.

Akizungumza mbele ya familia ya Mtemi Milambo mbunge huyo alisema viongozi wengi wamekuwa wakiahidi kuboresha mazingira ya Makumbusho hayo lakini wameshindwa kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mambo ya kisiasa.

Kadutu alibainisha kuwa eneo hilo la Makumbusho linapaswa kuboreshwa ili lilingane na hadhi ya Mtemi Milambo tofauti na ilivyosasa eneo hilo haliendani na heshima ya Mtemi huyo maarufu.

Aidha alizitaka serikali kuu na halmashauri ya wilaya ya Kaliua zianze kutambua na kuona umuhimu wa kuwaenzi watemi mbalimbali ambao waliongoza mapambano ya kupinga ukoloni.

Mbunge huyo alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuungana kwa pamoja ili kutimiza azma ya kuboresha mazingira yanayozunguka Makumbusho ya Mtemi Milambo pamoja na watemi wengine waliomtangulia.

Mheshimiwa Kadutu alianisha baadhi ya faida zitakazojitokeza baada ya kuliboresha eneo hilo kuwa ni kuwavutia wageni wengi zaid wa ndani na nje ya Tanzania kufanya utalii ambao utakuza uchumi na kutoa ajira kwa wakazi wa jimbo la Ulyankulu.

Awali akisoma taarifa ya Makumbusho hayo afisa tarafa wa tarafa ya Ulyankulu John Chitanda alisema jamii inayoishi kuzunguka makumbusho hayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa shule, zahanati, barabara na visima virefu vya maji.

Eneo la Makumbusho ya Mtemi Milambo lipo katika eneo la kijiji cha Usigala barabara ya 44 katika jimbo la Ulyankulu na mtemi huyo alifariki mwaka 1884.

Friday, 11 December 2015

JE WAJUA? SIRI YA UTEMI KATIKA FAMILIA YA MTEMI MILAMBO?




Na Paul Christian,Ulyankulu.

Mzee Solomoni Kazwika Milambo ni mmoja wa wazee wachache wa ukoo wa Mtemi mashuhuri Milambo ambaye anaishi katika kijiji Usigala barabara ya 44 Ulyankulu mkoani Tabora.

Kijiji hicho cha Usigala kipo kwenye eneo ambalo linajulikana kama Ikonongo wakati wa utawala wa Mtemi Milambo.

Mzee huyo amezaliwa siku ya Jumatatu asubuhi ya tarehe 18, Julai mwaka 1945 na sasa ametimiza umri wa miaka 70.

Mnamo tarehe 28 Novemba, 2015 mzee Solomoni anakutana wa jopo la waandishi wa habari na kufanya mahojiano maalum kuhusu  sifa za mtu anayepewa Utemi katika ukoo wa Mtemi Milambo. 

Mzee huyo alisema, “Sisi kupewa Utemi inatokana na jinsi mtu alivyozaliwa au unabii unasemaje kuhusu mtu huyo.”

Alisema katika ukoo wa Milambo kabla ya Milambo hajazaliwa alianza Sibuga ambapo alipozaliwa ilishuka nyota moja, babu yake na Milambo aliyejulikana Kasele Muhofu aliongea akiwa bado tumboni mwa mama yake na ndio maana aliishi miaka 300, (1520-1820).

Mzee Solomoni alifafanua, “halafu alifuata shangazi Kibete alizaliwa akiwa malkia mwenye ziwa “titi moja” la mkono wa kushoto.”

“Mimi mwenyewe kabla ya kuzaliwa niliongea nikiwa tumboni mwa mama yangu na sikunyonya maziwa ya mama.” Aliongeza mzee huyo.

Mzee Solomoni alibainisha kuwa katika ukoo wa Milambo, mtu anayekabidhiwa mikoba ya Utemi ni lazima azaliwe kimaajabu au kuwe na unabii juu yake.

Alifafanua kuwa ikitokea akasimikwa Utemi mtu asiyetokana na maajabu au maelekezo maalumu hawezi kumaliza miezi miwili au mitano.

Siku hiyo ya Novemba 28, 2015, mzee Solomoni aliongoza jopo la wazee wa ukoo wa Milambo katika zoezi la kimila la kumsimika mbunge wa jimbo jipya la Ulyankulu John Peter Kadutu kuwa Mtemi.

Akizungumzia tukio hilo mzee huyo alisema kabla ya kumsimika mheshimiwa Kadutu nilioteshwa namna ya kumfanyia hivi na vila na kama nisingeoteshwa leo mvua isingenyesha.

Mzee Solomoni aliongeza “ndio maana mvua ilianza kunyesha kuanzia saa tatu asubuhi hadi muda ule tunafanya tambiko la kimila la kumsimika mheshimiwa Kadutu.”

PADRI ANTONY KATOBA:KANISA KATOLIKI LA BARABARA YA 13 ULYANKULU LIMEJENGWA KWENYE ARDHI YA ILIYOKUWA IKULU YA MTEMI MILAMBO




Na Paul Christian, Ulyankulu.

Paroko wa Parokia ya Kanisa Katoliki Ulyankulu Padri Antony Leonard Katoba amesema eneo lilipojengwa Kanisa Katoliki barabara ya 13 Ulyankulu,mkoani Tabora ni la kihistoria kwa kuwa ndipo ilipokuwa Ikulu ya pili ya Mtemi Milambo.

Amesema Ikulu hiyo ya Mtemi Milambo ilijulikana kwa jina la Iselamagazi na ilianza kujengwa mwaka 1879 na kukamilika mwaka 1883.

Padri Katoba anabainisha kuwa Ikulu hiyo ya Iselamagazi ilitumiwa na Mtemi Milambo kiutawala na pia ilikuwa kambi ya jeshi la Mtemi Milambo lililojulikana kama “Walugaluga”.

Aidha Paroko huyo ameeleza kuwa Mtemi Milambo alikuwa na Ikulu nyingine Ikonongo ambapo ndipo yalipokuwa makazi ya Mtemi huyo mashuhuri.

Padri Katoba anasema, “Mtemi Milambo alianza kuijenga Ikulu ya Ikonongo mwaka 1880 na kuikamilisha mwaka 1883.”

Paroko huyo wa Parokia ya Ulyankulu amesema Kanisa Katoliki lilikabidhiwa eneo hilo mwaka 1975 kwa ajili ya kulilinda na kulitunza na kwamba wanaendelea kulitunza na kulienzi.


Wednesday, 9 December 2015

John Kadutu:Ulyankulu ni lazima ikimbie kiuchumi



HOTUBA YA MH. JOHN PETER KADUTU MBUNGE WA ULYANKULU ALIYOITOA TAREHE 28 NOV, 2015 KWENYE VIWANJA VYA KANISA KATOLIKI PAROKIA YA ULYANKULU BARABARA YA 13.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!
 
We DJ usije kuleta maneno hapa.Najua watu wanataka nipige show, naweza nikapiga hapa ikawa shida.

Mheshimiwa mwenyekiti wa CCM wa wilaya Mzee wetu, mzee Kaseko, 

Mheshimiwa Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa kaka yangu Professor Kapuya,

Wajumbe wa kamati ya siasa wa mkoa wa wilaya,

Waheshimiwa Madiwani wenzangu,

Waheshimiwa Wazee, Vijana, Kinamama na Akinamama,

Mtumsifu Yesu Kristo, Asalam Aleykhum.

Kwanza nimshukuru mwenyezi mungu kutufikisha leo, siku nzuri, siku tuliyovumilia pamoja na mvua. Tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu.

Lakini niwashukuru wananchi wote kwa kufika, tena kwa uvumilivu mnanionyesha mnanipenda kweli kweli na mimi ninaona nina deni Bado.Nawashukuruni sana.

Lakini pia niishukuru familia ya mtemi Milambo, jamani leo nimekabidhiwa jambo hili kubwa niko vizuri hapa ukileta mambo ya Ndumba Nangai nakushughulikia.

Mkitaka turudi kwenye uchaguzi nitumie Ndumba Nangai za Milambo mtapata shida,wale watoto wa mama mdogo.

CCM Oyeeeee!!!!!! Ulyankulu Oyeeee!!!!!

Wazee wangu nawashukuruni sana kwa kunipa heshima, ni heshima kubwa, inayohitaji kuwatumikia wanaUlyankulu kwa moyo thabiti.

Ndugu zangu wanaUlyankulu, Niwashukuru kwa imani kubwa mlioionyesha wakati wa uchaguzi mkuu.Mmenipa nguvu, ushindi wa asilimia 75 na ushee si haba.

Lakini pia ushindi aliopata mheshimiwa Magufuli kwenye jimbo letu ni wa kujivunia,kama sio wa kwanza kimkoa basi wa pili kimkoa,Ninaimani ni wa kwanza kimkoa.Sijawasikia wengine,hii ni jinsi gani imani tuliyonayo.

Mheshimiwa Magufuli amepata asilimia za kitaifa 58 za kwetu 81 na ushee kwa hiyo utaona tuliochangia kuifikisha 58 mojawapo ni Ulyankulu.Tupaswa kujipongeza sana.

Lakini kwa niaba yake,nawashukuruni sana kwa jambo hilo,pia niwashukuru wapiga kura wote wa jimbo letu kwa kuwachagua madiwani, tena wote wa Chama Cha Mapinduzi.

Kwenye jimbo letu madiwani wote asilimia 100 ni wa Chama Cha Mapinduzi. Kwa hiyo mchango wetu kwenye Halmashauri ya wilaya ya Kaliua, sisi tunatoka tukiwa asilimia 100.Nawashukuruni sana kwa imani hiyo.

Mmekionyesha Chama kokote hadi ngazi ya Taifa kwamba chama cha Mapinduzi kinaaminiwa. Asanteni Sana.

Ndugu zangu uchaguzi umekwisha, na ndio maana leo hapa hatusemi semi vijembe.Ndio maana nimewaambia leo sipigi SHOW.

Maana yake wakati wa Uchaguzi kuzitafuta kura, ilibidi nipige show ili watu waone kama tuko vizuri. Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!

Uchaguzi umekwisha na sasa kazi tu. Jimbo letu la Ulyankulu tunahitaji kukimbia, nilikuwa nikiiwaambia wakati wa kampeni tunataka maendeleo ya haraka, tunautaka mchakamchaka.
Kwa bahati njema, wananchi wa jimbo letu la Ulyankulu ni wachapakazi. 

Sasa baada ya kuwa na jimbo tusirudi nyuma,tukadhani jimbo litafanya kila kitu.Niwasihi na niwaombe sana ndugu zangu wa Ulyankulu sasa tuchape kazi kweli kweli.

Tuchape kazi ili maendeleo yetu ya jimbo hili la Ulyankulu yaende haraka haraka.Na hasa kwa kuwa tuko mbioni kutafuta Wilaya na Halmashauri,ili mambo haya yatakapo tufikia twende mbio. 

Tunahitaji uchumi uwe mzuri ndani ya jimbo letu.Tunahitaji kuboresha maisha ndani ya jimbo letu.

Tunahitaji kuboresha huduma za afya.Tunahitaji Elimu, miundombinu ya barabara na mawasiliano.

Lazima tufanye kazi.Lakini ndani ya Ulyankulu ya Makazi kazi nyingi zilifanywa na UN, baada ya kuwa mmepata uraia ndugu zangu sasa kazi.

Kwingine kote maendeleo yanaletwa na wananchi wenyewe,hivyo tuanze kubadilika sasa kujua kwamba tunahitaji kuchangia maendeleo  kuanzia vijiji, kata na hadi kupata wilaya.

Lazima tuhakikishe tunafanya kazi kwa maana ya kuchangia Maendeleo,ili jimbo letu liwe mstari wa mbele na maendeleo yake yaonekane.

Nawajua watu wa Ulyankulu,sisi sio wavivu, niwachapa kazi. Tuongeze kilimo cha tumbaku. 

Huko nyuma SES kwa maana ya ushuru wa Tumbaku ndani ya makazi haukuwa unarudi kusaidia maendeleo, kwa hiyo sasa tuongeze juhudi kwa kilimo cha tumbaku, pamoja na shida zake.

Tulisema wakati wa kampeni tunaungana wabunge wote wa mkoa, tuhakikishe tunashughulika na zao la Tumbaku ili liboreshwe, ili mapato yajulikane, pembejeo zije kwa wakati.

Lakini masoko yawepo, bei ziboreshwe, kazi hiyo wabunge wenu wa mkoa wa Tabora tutaifanya muda si mrefu.

Tunataka masoko ya Tumbaku angalau mawili kwa mwezi,sio soko moja kwa miezi miwili, mitatu.

Hatutaki fedha za Tumbaku zije wakati masika imefika.Tunataka fedha ya Tumbaku ije mapema. Lakini tunataka usimamizi wa zao kwa ujumla tushughulike nao.

Kwa hiyo tutaongea na wenzetu wa Ushirika, Bodi ya Tumbaku, na wadau wote wanaohusika na Tumbaku. 

Kwa nini nalisema hili.

Tumbaku ndio zao linaloingiza fedha za kigeni katika mazao ya kilimo.Lakini Tumbaku hiyo hiyo inatoka nyingi Ulyankulu. Lazima tumbaku itusaidie kuboresha maisha yetu.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!

Kwa hiyo ndugu zangu nataka tuongeze spidi ya kilimo lakini juu ya mazao mengine mahindi, maharage, alizeti idara ya ushirika itatusaidia.

Na nina uhakika muda si mrefu mashine za kukamua alizeti zitapatikana.Alizeti, wenzetu wa Singida sasa ni zao linalowasaidia na maisha yanakwenda  pamoja na kwamba eneo lao linaukame.

Lakini kama nilivyosema,ahadi nyingi tumezitoa ni ahadi za miaka mitano.Baada ya kumaliza uchaguzi kumekuwa na shida, watu wakaanza kufikiri kesho yake tu, tunaanza kutekeleza  ahadi, kuna watu wakaanza kuniuliza ulisema maji mbona hatujaona hata mitambo.

Jamani ahadi hizi ni za miaka mitano, tutajitahidi, serikali kwa upande wake itafanya inaloweza. Lakini ziko ahadi za mbunge tutatekeleza moja baada ya nyingine, na tumeanza kutekeleza.

Tumeanza kutekeleza, nikuaambieni ikifika mwaka wa nne nataka asilimia 95 ya utekelezaji wa hizi ahadi uwe umefanyika.

Nikuambieni mimi ni kazi tu. Na tumeanza.

Shida za maji tutahakikisha tunalifanyia kazi, barabara tutafanyia kazi, ziko kazi za binafsi, ziko kazi zitafanywa na TANROAD, ziko kazi zitafanywa na Halmashauri.

Tunauhakika baada  ya miaka mitano serikali ya Chama Cha Mapinduzi itakuwa imetekeleza. 
 
Bila shaka kila mmoja amesikia kazi imeanza huko, watu wanafurushwa sasa , eeeh ukizubaa kesho anakuja anaibuka tu, ziara ya ghafla na mimi nitazifanya ziara za ghafla.

Nataka nitume salamu kwa watumishi ndani ya jimbo letu, mpo mnanisikia, watumishi wote ndani ya jimbo tunataka kazi,achaneni na siasa,tunataka mtufanyie kazi. 

Mtoe huduma kwa wananchi kwa wakati. Kwa sababu sisi wengine tutafanya kazi mashambani, kila sehemu biashara,tunataka wafanyakazi ndani ya jimbo letu wafanye kazi inayoonekana. 

Na tutaiagiza serikali. Alikuwepo hapa mkuu wa wilaya, alikuwepo Mkurugenzi.Tunataka wafanyakazi wa jimbo letu wachapekazi. Sio kuwa mwanzo wa matatizo,  sio kukaa vijiweni,sio kushughulika na siasa.Siasa tuachieni akinaKadutu na wengine.

Ulyankulu Oyeee!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa hiyo ndugu zangu, leo sherehe yetu hii ilikuwa ni kujipongeza lakini kuanza kuona kwamba tunataka kufanyanini. Tunayo mambo mengi mno ya kufanya.Lakini jambo moja niwaambie basi.

Ndio maana niliwaambia sisi utekelezaji unaanza mara moja tumefuatilia na baadae tumefanikiwa, kusajili kata tatu za Ulyankulu. Nilikuambieni niachieni mi ndio najua njia.

Tumeisha pata kata tatu, sasa tunaisubiri tume ya uchaguzi itapanga utaratibu wa uchaguzi, ndani ya kata zetu tatu za ulyankulu. 

Lakini ninauhakika tutaendelea kuomba kata ziongezwe hasa eneo hili la Makazi Ulyankulu ili tuwe na kata nyingi za kutosha.

Ni imani yangu tukipata kata mambo yatakwenda vizuri.

Ulyankulu Oyeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa hiyo ndugu zangu muda na wenyewe umetutupa hatuna maneno mengi zaidi ya kuwashukuru lakini nataka kukuambieni tumeisha anza kazi na nitapita kijiji kwa kijiji, kuhakikisha ahadi ambazo tumezitoa tunaanza kutekeleza.

Kuna ahadi kwa mfano tumetoa kwa ajili ya mifuko ya simenti ya zahanati, tunaanza Disemba hii kutoa simenti kwa zahanati.Nia yetu ni kuhakikisha watu wanapata huduma ya afya ili kazi za maendeleo zifanyike na kadhalika.

Lakini kabla sijamaliza nimshukuru kwa dhati kaka yangu Professor Kapuya, kwa dhati kabisa, Profesor amekuwa msaada kwangu kabla ya kupata ubunge na sasa na hata leo mnavyomuona hapa ametoka Dar es Salaam kwa ajili ya shughuli hii tu.

Akimaliza hapa anarudi zake Dar es Salaam. Kaka Ebu Njoo Useme Kidogo………

HOTUBA YA PROFESSOR  JUMA KAPUYA.

CCM Oyeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kadutu Oyeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Unajua wahenga walisema kuzaa sio kazi ila kulea ndio kazi, lakini nataka niwaambie mimba nyingine zinasumbua mimba ya kuizaa Ulyankulu ilikuwa kazi, lakini na hatimaye nikazaa nawapongezeni sana.

Sasa hii ndio Tanzania tunabadilishana uongozi huku tunacheka,Kadutu nimemlea namfahamu ni jembe ninawaacha katika mikono salama. Mikono yenye uchu wa maendeleo. 

Na kama mlivyomsaidia kwa kupata timu ya madiwani ambao wote wanatokana na Chama Cha Mapinduzi,sasa kazi tu.

Maana yake hatokuwa na vikwazo vikwazo anapojadiliana na wenzake juu ya maendeleo katika eneo letu la Ulyankulu. 

Nataka niwahakikishieni, kwamba tutafanya kila tunaloweza kuendelea kushikamana na Kadutu na madiwani hawa ili yale ambayo yamebaki tuyakamilishe.

Malengo yetu ni kuhakikisha wilaya inapatikana, Halmashauri inapatikana ili kwa kufanya hivyo kiwe ni kichocheo sasa cha maendeleo kweli kweli.

Kila kiongozi mwenye busara anapenda maeneo ya utawala yawe madogo ili kusogeza huduma. 

Kiongozi ambaye hana busara anang’ang’ania maeneo makubwa ya utawala ili wananchi waendelee kuteseka.

Mimi na Kadutu hatuko hivyo. 

CCM Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!

Kaka Kadutu, nashukuru kwa kunipa nafasi kuzingumza na wananchi.

Nataka niwahakikishieni nami nitakuwa nakuja mara kwa mara, naipenda Ulyankulu yote, naipenda Makazi, na ikiwezekana mnitafutie tafutie na kakiwanja hivi ,nami nihangahike hangahike kuwa muwekezaji mdogo mdogo, mjasiriamali. 

Kwa hiyo madiwani mnapokaa huko mnifikirie fikirie kaeneo ili na mie niwe mjasiriamali mdogo mdogo hivi.

CCM Oyeeee !!!!!!!!!!!!!!,       Kadutu Safiii!!!!!!!!!!!!!!!

…………………HOTUBA YA MHESHIMIWA JOHN PETER KADUTU

Eeeeee huyo ndio Kapuya bwana.Nimelisema hili, kaka yangu ameanza kunisaidia mnayo habari tumekwisha kuanza vikao vya bunge,Kisha anza kunionyesha njia, ukienda pale, yule atakusaidia, ukienda kwa huyu katibu atakusaidia.

 kazi hiyo Kapuya kisha anza kuifanya. Na nimeanza kuwa mwenyeji bungeni.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Eee unajua ukikuta wenyeji wazuri, basi huimgeni,mambo yanakwenda vizuri. Lakini niseme tena SITAWAANGUSHA. Januari tunaanza shughuli mtaishuhudia.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Si mnaijua, nataka kuwa king’ang’anizi huko, nyie muda ukifika kaeni huko muwe mnachungulia,halafu shughuli itakuja.

Ndugu zangu naomba niwatambulishe sasa, Lufungija njoo,Chatanda ukae, huyu afisa tarafa alitaka kuacha kazi yake awe katibu wa mbunge, sasa nimemwambia yeye akae tu. 

Jamani huyu mdogo wangu mheshimiwa Jafael Lufungija ndiye katibu wa mbunge kuanzia leo. 

Huko nyuma alikuwa anaratibu, sasa leo kulitokea mkanganyiko kati ya afisa tarafa na  yeye, nani katibu wa mbunge, sasa huyu ndio katibu wa mbunge.

Ebu wasalimie bwana…………………………………………………

HOTUBA YA JAFAEL LUFUNGIJA.

Ulyankulu Oyeeeeee!!!!!!     Kadutu Oyeeeee!!!!!!!!

Mheshimiwa mwenyekiti wa sherehe hii,

Waheshimiwa wageni waalikwa Mabibi na Mabwana,

Mheshimiwa mbunge wetu mtaafu Juma Kapuya,

Na viongozi wote wa chama cha Mapinduzi na wasio wa Chama Cha Mapinduzi,
Asalam Aleykhum,tumsifu yesu kristo,   
                                           
Ndugu zangu kwa majina naitwa Lufungija, Nimepewa kazi rasmi leo ya kuteuliwa kuwa katibu wa mbunge mheshimiwa John Peter Kadutu kwa imani ya kuniamini kufanya shughuli zako katika jimbo hili.

Lakini ni wahakikishie ndugu zangu wananchi, viongozi na wanachama wote na wasio wananchama wa Chama Cha Mapinduzi nitatenda haki katika shughuli za kumsaidia Mheshimiwa mbunge bila kubagua chama, bila kubagua rangi wala Utajiri. 

CCM Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Nitahakikisha Mheshimiwa Mbunge nampelekea taarifa sahihi, nitahakikisha mheshimiwa Mbunge namshauri vizuri kwa maendeleo ya jimbo la Ulyankulu. 

Ulyankulu  Oyeeeeeee!!!!!!!!!!!!

Niwahakikishie ndugu zangu, mheshimiwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wa kata ya Ilege na wanaIlege wote msiwe na hofu Ilege itasonga mbele, lakini wana Ulyankulu msiwe na hofu jimbo la Ulyankulu Litasonga mbele.

Viongozi wote wa ngazi za kata nitahakikisha kila Halmashauri, na WDC nawatembelea kwa maana ya kwenda kusikiliza kero za wananchi ili kumfikishia mheshimiwa mbunge taarifa zilizosahihi.

Sitafanya shughuli za kuwabaguwa wala sitampelekea taarifa za majungu. Niwaombe ndugu zangu viongozi wa Madhehebu na Makundi mbalimbali.

Naomba tupeane ushirikiano na niwahakikishie nitayatendea haki madhehebu yote kama nilivyoeleza nitatenda haki katika kata zote.

Ulyankulu Oyeee!!!!!!!!!!!!!                 CCM Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mheshimiwa Kadutu, nakuhakikishia hapa kazi tu.

Na mimi nitakushauri sitaogopa uteuzi wako, unajua kazi za kuteuliwa unaweza kuwa unaogopa ogopa. Kwa hiyo nitakushauri ukweli bila kuogopa kazi ya Uteuzi.

 Ulyankulu Oyeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!   CCM Oyeeeee!!!!!!!!!

Nawashukuru sana Asanteni Sana.

…………………………HOTUBA YA MHESHIMIWA JOHN PETER KADUTU

Niliacha kidogo kutoa shukurani kwa kamati ya kampeni, sijui mpo, kamati ya kampeni ya Jimbo Asante, lakini kipekee nimshukuru mdogo wangu mheshimiwa Kitogoli diwani mstaafu upo!!!

La mwisho ndugu zangu watu wa Ulyankulu zipo alama za ubaguzi, zipo alama za ubaguzi, naomba tuzikemee kumekuwepo na dalili za ubaguzi watu wanasema huyu Msukuma, huyu Mnyamwezi, huyu Mhutu. 

Naomba Tuzikemee.Tunataka kuijenga Ulyankulu yenye umoja, Ulyankulu isiyokuwa na ubaguzi.

Huyu ndio mheshimiwa Kitogoli tulipambana hapa wakati wa kampeni ….. Ah maneno mengi sana huyu.

Ebu salimia wakumbuke kumbuke sauti yako.

HOTUBA YA MHESHIMIWA MOSHI KITOGOLI

CCM Oyeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!! 

Jamani mbona leo mnaniangusha mmechoka, naomba muonyeshe furaha kwa mheshimiwa Kadutu, tunyooshe mikono tafadhali, CCM Oyeeee!!!!! Kadutu bomba si bomba.

Kwa majina, kuna watu ambao hamnifahamu naitwa Moshi Kitogoli ndiye mwenyekiti wa umoja wa Vijana wa CCM wilaya ya Kaliua lakini pia ndiye nilikuwa mpambanaji kuhakikisha tunapata ushindi wa kishindo kama huu.

Lakini zaidi ya yote ndugu zangu wa Ulyankulu naomba nichukue nafasi hii, najua brother hawezi kunikataza, kwa sababu anajua ninalolisema ni jema sana.

Ndugu zangu tunawashukuru sana,tulikuja na misemo mbalimbali mkatuelewa na mwisho tarehe 25 mkafanya kweli, tunawashukuru sana Ulyankulu, Mungu awabariki aendelee kuwalinda awape afya njema ili keshokutwa tukija kushambulia kwenye kata hizi tatu, tuonyeshe ushindi mwingine wa kishindo zaidi. 

CCM Oyeeee!!!!!!!!!!

Niliwaambia siku ile hapo kwamba mheshimiwa Kadutu anakuja na upepo mzito,watu katika hali ya kawaida mmezoea ule upepo unaitwa vimbunga, sijui sunami,lakini mimi nikawaambia kuna upepo kabambe unaitwa ikunula.

Upepo huu ni balaa,utahakikisha unang’oa mpaka mizizi na mimi nakubaliana na nyinyi kwamba siku ile mliniahidi ule upepo mpya mnauona kishindo chake.

Naamini hapa ndani Moleka kaka yangu ameniambia anasema hao watu hawawezi kuweka mguu, endelea kunywa maji yatelemke tunasubiri kibali, kaka Kadutu atakileta. Tuhakikishe kata zote tatu zilizobaki tunashinda CCM.

CCM Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!! Asanteni Sana.

……………………………….HOTUBA YA MHESHIMIWA JOHN PETER KADUTU

Eeh huyu tulikuwa tunamtanguliza wakati wa kampeni anapiga, anapambana na yale maneno yakifedhuli fedhuli. Na siku nyingine nitamleta, Nimeshaona ni dawa. 

Lakini nataka niwakumbushe baada ya uchaguzi kwisha madiwani walioshinda, mbunge wenu, na Rais ni viongozi wanawatumikia wananchi wote,bila kujali itikadi.

Niwakaribishe sana ndugu zangu wa CHADEMA, CUF, ACT tuungane kwa ajili ya maendeleo ya Ulyankulu. Itikadi zetu tuziweke pembeni kwa sababu ya maendeleo. 

Baada ya kusema hayo ndugu zangu naomba nifanye kazi moja. Mimi ni mtu wa michezo kila nilimotembea niliahidi kutoa jezi pamoja na mipira.

Leo ninayomafurushi yako kwenye lori pale.Vijiji vyote vinapata jezi na mipira. HAPA KAZI TU.

Ulyankulu yote itavaa jezi mpya na mipira mipya. Tumeanza na michezo. Lakini muda si mrefu mtaona tunashughulika na visima, tunashughulika na maji kabla ya serikali kuleta pesa.

Tunataka kutumia hizi hizi posho, posho hizi hizi za Mbunge zianze kufanyakazi kabla ya pesa ya serikali haijaja. Pesa ya serikali itatukuta tupo njiani tunaendelea, ndio kazi ya maendeleo hatutaki bla bla.

Tunataka tuwe mbele kuliko wengine. Na ninaimani nikuambieni Halmashauri inakuja, Wilaya inakuja na niwadokeze Mheshimiwa Majaliwa lilipotajwa jina lake tunaelekea kupiga kura kumpitisha Bungeni nilinong’onezana naye. 

Basi hizo ndio kazi zangu kupenya.Lazima uwe na kiongozi mjanja. Nimezaliwa Ichemba lakini mimi mtoto wa mjini.

Ulyankulu Oyeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!

Mheshimiwa Majaliwa alikubali, atakuja siku moja kutembea Ulyankulu. Tuendelee kumuombea kazi ni nzito ile, lakini iko hazina moja kwa mheshimiwa Majaliwa anayajua maeneo yote alivyokuwa Urambo pamoja na Ulyankulu. 

Tena akaniuliza barabara ya 13 pakoje, nikamwambia pamechangamka sana siku hizi.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!

Sasa ndio salamu tunaendelea kupenya siku moja nitawaambia tumepenya vipi. Kazi yangu itakuwa kuleta taarifa hapa za bungeni kabla na baada.

Tutatafuta utaratibu ili mjue tunafanya nini na tutatoa taarifa kila wakati kwenye mikutano ili kila mwananchi ajue.

Lakini jambo lingine ni juu ya Chama Chetu cha Mapinduzi, lazima tukiimarishe chama chetu cha Mapinduzi kwa ajili ya uchaguzi ujao wa mwaka 2020.

Lazima tuhakikishe tunajenga ofisi za matawi na kata kwenye maeneo yetu. Hiyo tutakuwa tumeimarisha chama chetu kiwe imara tusipate tabu.

Lakini kubwa nimeisha zungumza na katibu wa wilaya dada yangu Neema Adamu anatayarisha utaratibu wa kuja kutoa semina kwa viongozi wote wa Matawi.

Mtakula na kulala ili watu wajue shughuli za chama zikoje.Tulipata tabu kidogo wakati wa Kampeni kukawa na shida watu hawajui hata hitifaki.

Sasa tunataka kuleta mafunzo kwa viongozi wote wa Matawi pamoja na Mabalozi ili kuhakikisha kila mmoja anajua wajibu wake lakini ili uchaguzi ujao wa mwaka wa 2020 tusipate tabu.

Tunataka 2020  Mbunge apate asilimia 99.9, Rais apate asilimia 100.

Najua kazi kubwa tuliyoifanya wenzetu wale waliondoka saa tisa za usiku kabla ya matokeo, tunajiandaa kwa mwaka 2020 kimbunga hicho kitakuwa kikali kuliko hiki.

Ulyankulu Oyeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!

Sasa waheshimiwa wananchi pamoja na viongozi nimalizie kazi hii, hii ni sampuli mafurushi yako kwenye lori.

Nimuombe  diwani mtarajiwa wa Milambo aje hapa halafu mbunge mstaafu atakuwa akiwapatia seti ya jezi.

Tabu tuliyonayo mbunge huyu mstaafu anamatatizo yeye ni Simba sana, sasa ameamua kumchagulia Moleka Jezi Nyekundu……………. Hivi vingine na Mpira utamuona katibu wa Mbunge.

Anayefuata diwani mtarajiwa wa Igombemkulu na diwani mtarajiwa wa Kanindo awe karibu, naomba mwakilishi wake.

Mwakilishi, Sasa upendeleo nani apewe, Haya Seleli, diwani wa Seleli mheshimiwa Buyobe. …………………….Tatizo anataka kuacha kugawa sababu ni za Yanga. 

Jamani hii ni Sampuli mzigo huko kwenye Lori pale, vijiji vyote vinapata, sawa!!!!

Lakini wakati huo huo tukijiandaa baada ya masika kuna mashindano yanakuja lakini kwa wakati huu nimekwisha zungumza na uongozi wa chama cha Mpira mkoa wanatuandalia wakufunzi wakuja kufundisha kwa ajili ya makocha pamoja na waamuzi wa Mpira.

Baada ya kusema hayo niwashukuru tena, nawashukuruni kwa kuja lakini kubwa nawashukuruni kwa kuniamini. 

NARUDIA SITAWAANGUSHA NDUGU ZANGU, ASANTENI SANA NA MBARIKIWE SANA, ASANTE.