Featured post

HABARI KATIKA PICHA: ZIARA YA KWANZA YA MBUNGE WA KWANZA WA JIMBO LA ULYANKULU JOHN PETER KADUTU

MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA DINI VIONGOZI WA DINI WAKIFUATILIA HOTUBA YA MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUT...

Saturday, 9 January 2016

HABARI KATIKA PICHA: ZIARA YA KWANZA YA MBUNGE WA KWANZA WA JIMBO LA ULYANKULU JOHN PETER KADUTU

MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI WA DINI
VIONGOZI WA DINI WAKIFUATILIA HOTUBA YA MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUTU
VIONGOZI WA DINI JIMBO LA ULYANKULU WAKIPIGA MAKOFI KUASHIRIA KUKUBALIANA NA HOTUBA YA MH. JOHN KADUTU
MH. JOHN KADUTU (ALIYESIMAMA) NA VIONGOZI WA DINI WA JIMBO LA ULYANKULU
KATIBU WA MBUNGE JAFAEL LUFUNGIJA AKIFUNGUA KIKAO CHA KAZI CHA VIONGOZI WA DINI PAMOJA NA MBUNGE JOHN KADUTU
NYUMBA PEKEE YA WAGENI KATIKA KATA YA ICHEMBA

MH. JOHN KADUTU AKIWASIKILIZA VIONGOZI WA VYAMA VYA MSINGI VYA USHIRIKA KUTOKA JIMBO LA ULYANKULU

WANAUSHIRIKA WA JIMBO LA ULYANKULU KATIKA KIKAO CHA KAZI PAMOJA NA MH. JOHN KADUTU KILICHOFANYIKA KWENYE UKUMBI WA RC BARABARA YA 13

VIONGOZI WA VYAMA VYA MSINGI VYA USHIRIKA ULYANKULU WAKITAFAKARI HOTUBA YA MH. JOHN KADUTU


MH. JOHN KADUTU (KATIKATI) AKIELEKEA KWENYE UKUMBI WA MIKUTANO WA CHUO CHA VETA ULYANKULU



MH. JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA CHUO CHA VETA ULYANKULU
JENGO LA UTAWALA LA CHUO CHA VETA ULYANKULU

UKUMBI WA MIKUTANO WA VETA ULYANKULU ULIZINDULIWA MWAKA 2005

KAIMU MKUU WA CHUO CHA VETA GOSBERT H. KIBANI AKISOMA TAARIFA YA CHUO HICHO KWA MH. JOHN KADUTU
WAKUU WA SHULE,WALIMU WAKUU, MAOFISA UGANI,WATUMISHI WA AFYA, WATENDAJI WA VIJIJI NA KATA WA JIMBO LA ULYANKULU  WAKIFUATILI HOTUBA YA MH. MBUNGE JOHN KADUTU

MH. JOHN KADUTU ( WA PILI KULIA) AKISIKILIZA MAONI, MAOMBI NA KERO ZINAZOWAKABILI WALIMU, WATUMISHI WA AFYA, MAOFISA UGANI NA WATENDAJI WA VIJIJI NA KATA

MBUNGE WA JIMBO LA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIWAHUTUBIA WAKUU WA SHULE, WALIMU WAKUU,MAOFISA UGANI,WATUMISHI WA AFYA, WATENDAJI WA VIJIJI NA KATA KUTOKA JIMBO LA ULYANKULU


WATAALAM WA SEKTA YA ELIMU, AFYA,KILIMO NA UTAWALA WA JIMBO LA ULYANKULU WILAYA YA KALIUA WAKIFUATILIA KWA MAKINI HOTUBA YA MH. MBUNGE JOHN KADUTU

MH. JOHN KADUTU AKIKAGUA JENGO LA UPASUAJI AMBALO LIMETELEKEZWA KWA MIAKA KADHAA ILIYOPITA KATIKA KITUO CHA AFYA CHA ULYANKULU

MUUGUZI WA KITUO CHA AFYA ULYANKULU FATUMA (KATIKATI) AKIELEZA UMUHIMU WA KUKAMILIKA KWA JENGO HILO 
MBUNGE WA ULYANKULU JOHN KADUTU AKIWA AMEMBEBA MTOTO MCHANGA KATIKA WODI YA WAZAZI KATIKA KITUO CHA AFYA ULYANKULU
MH JOHN KADUTU AKIKAGUA JENGO LA UPAUSUAJI AMBALO UJENZI WAKE UMESIMAMA KWA MUDA MREFU
BAADHI YA WATUMISHI WA KITUO CHA AFYA ULYANKULU WAKIMSIKILIZA MH. JOHN KADUTU

MH. JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA ASKARI WA KITUO CHA POLISI ULYANKULU

ASKARI WA KITUO CHA POLISI ULYANKULU WAKIFUATILIA HOTUBA YA MBUNGE MH. JOHN KADUTU

GARI LA KITUO CHA POLISI ULYANKULU LINAHITAJI MATENGENEZO BAADA YA KUHARIBIKA KWA AJALI
MKAZI WA KIJIJI CHA ICHEMBA TARAFA YA ULYANKULU AKIJIANDAA KWENDA SHAMBA
GARI LILILOTUMIKA KUMBEBA MBUNGE WA ULYANKULU MH. JOHN KADUTU WAKATI WA ZIARA YA SIKU TATU (JAN 5 HADI JAN 7 2016) YA KUTEMBELEA TAASISI ZA UMMA NA BINAFSI ZILIZOMO KATIKA JIMBO HILO

MH. JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI YA MKUU WA MAKAZI ULYANKULU ILIYOPO BARABARA YA KWANZA

MWAKILISHI WA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KALIUA, AFISA UTAMADUNI NA MICHEZO MARKO KAPELA AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA  WATUMISHI WA OFISI YA MKUU WA MAKAZI ULYANKULU

MH. JOHN KADUTU AKISAINI KITABU CHA WAGENI KWENYE OFISI YA MKUU WA MAKAZI ULYANKULU

MH. JOHN KADUTU (SUTI) AKITETA JAMBO NA MWANDISHI WA HABARI WA MAGAZETI YA HABARI LEO NA DAILY NEWS MKOANI TABORA LUCAS RAPHAEL

MH. JOHN KADUTU (SUTI) AKIBADILISHANA MAWAZO NA KATIBU WAKE JAFAEL LUFUNGIJA

MH. JOHN KADUTU (SUTI) AKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA WATUMISHI WA KANDA YA KUSINI WA PORI LA AKIBA LA KIGOSI MOYOWOSI KATIKA KIJIJI CHA UHINDI

MH. JOHN KADUTU (KATIKATI)AKITETA JAMBO NA DIWANI WA KATA YA UYOWA ALPHONCE MSANZYA

MBUNGE WA JIMBO LA ULYANKULU MH. JOHN KADUTU AKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI YA PORI LA AKIBA LA KIGOSI MOYOWOSI KANDA YA KUSINI


Sunday, 13 December 2015

IJUE:HISTORIA FUPI YA MTEMI MILAMBO




Mtemi Milambo alizaliwa mwaka 1820 eneo lililojulikana kwa jina la Ikonongo na alipewa jina la Mbula Kasanda. 

Baba yake mzazi na Mtemi Milambo aliitwa Kasanda na mama yake alijulikana kwa jina la Mwasi Mpela.

Babu yake na Mtemi Milambo aliyejulikana kwa jina la Kasele Muhofu na ambaye aliishi miaka 300 baada ya kuzaliwa mwaka 1520 na kufariki mwaka 1820 alimrithisha utemi mjukuu wake Mbula Kasanda (Milambo).

Babu yake Mtemi Milambo, Kasela Muhofu kwa maajabu aliongea akiwa tumboni mwa mama yake kabla ya kuzaliwa na baada ya kuzaliwa hakunyonya maziwa ya mama yake.

Mbula Kasanda (Mtemi Milambo) kabla ya kutawazwa kuwa mtemi alitanguliwa na watemi tisa wa kwanza akiwa Sibuga aliyetawala kuanzia mwaka wa 22BK akafuatiwa na Mkindo wa Kwanza ambaye alirithiwa na Mlowa na kisha kufuatiwa na Moto wa Tatu.

Moto wa Tatu alirithiwa na Nsimba Nchembe ambaye naye alimwachia utawala Kapaya aliyerithiwa na Kasele Muhofu ambaye alimuachia utawala Kasimana Kasele.

Kasimana Kasele alikabidhi utawala kwa Mkindo wa Pili ambaye alimrithisha Mbula Kasanda maarufu kama “Mtemi Milambo.”

Mtemi Milambo alianza kutawala mwaka 1838 katika eneo la Ikonongo huku akiwa na Ikulu mbili za Ikonongo na Iselamagazi.

Kabla ya kifo chake kilichotokana na homa kali, Mtemi Milambo aliacha urithi wa kiti cha utemi kwa mtoto wake wa kike aliyejulikana kwa jina la Kibete mnamo mwaka wa 1884.

Kibete alizaliwa akiwa na ziwa moja yaani titi moja la mkono wa kushoto.

Kabla ya Kibete kufariki alikabidhi kiti cha utemi kwa Solomoni Kazwika Milambo ambaye alizaliwa siku ya Jumatatu asubuhi ya tarehe 18 Julai, 1945 ambaye yupo hadi hivi sasa.

Solomoni Kazwika Milambo kabla ya kuzaliwa aliongea akiwa tumboni mwa mama yake na hakunyonya maziwa ya mama yake.

 

KADUTU: “NITASIMAMIA UBORESHAJI WA MAKUMBUSHO YA MTEMI MILAMBO”




Na Paul Christian, Ulyankulu.

Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani Tabora Mheshimiwa John Peter Kadutu ameahidi kuboresha mazingira ya makumbusho ya Mtemi Milambo yaliyopo katika eneo la Ikonongo.

Akizungumza mbele ya familia ya Mtemi Milambo mbunge huyo alisema viongozi wengi wamekuwa wakiahidi kuboresha mazingira ya Makumbusho hayo lakini wameshindwa kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mambo ya kisiasa.

Kadutu alibainisha kuwa eneo hilo la Makumbusho linapaswa kuboreshwa ili lilingane na hadhi ya Mtemi Milambo tofauti na ilivyosasa eneo hilo haliendani na heshima ya Mtemi huyo maarufu.

Aidha alizitaka serikali kuu na halmashauri ya wilaya ya Kaliua zianze kutambua na kuona umuhimu wa kuwaenzi watemi mbalimbali ambao waliongoza mapambano ya kupinga ukoloni.

Mbunge huyo alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuungana kwa pamoja ili kutimiza azma ya kuboresha mazingira yanayozunguka Makumbusho ya Mtemi Milambo pamoja na watemi wengine waliomtangulia.

Mheshimiwa Kadutu alianisha baadhi ya faida zitakazojitokeza baada ya kuliboresha eneo hilo kuwa ni kuwavutia wageni wengi zaid wa ndani na nje ya Tanzania kufanya utalii ambao utakuza uchumi na kutoa ajira kwa wakazi wa jimbo la Ulyankulu.

Awali akisoma taarifa ya Makumbusho hayo afisa tarafa wa tarafa ya Ulyankulu John Chitanda alisema jamii inayoishi kuzunguka makumbusho hayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa shule, zahanati, barabara na visima virefu vya maji.

Eneo la Makumbusho ya Mtemi Milambo lipo katika eneo la kijiji cha Usigala barabara ya 44 katika jimbo la Ulyankulu na mtemi huyo alifariki mwaka 1884.

Friday, 11 December 2015

JE WAJUA? SIRI YA UTEMI KATIKA FAMILIA YA MTEMI MILAMBO?




Na Paul Christian,Ulyankulu.

Mzee Solomoni Kazwika Milambo ni mmoja wa wazee wachache wa ukoo wa Mtemi mashuhuri Milambo ambaye anaishi katika kijiji Usigala barabara ya 44 Ulyankulu mkoani Tabora.

Kijiji hicho cha Usigala kipo kwenye eneo ambalo linajulikana kama Ikonongo wakati wa utawala wa Mtemi Milambo.

Mzee huyo amezaliwa siku ya Jumatatu asubuhi ya tarehe 18, Julai mwaka 1945 na sasa ametimiza umri wa miaka 70.

Mnamo tarehe 28 Novemba, 2015 mzee Solomoni anakutana wa jopo la waandishi wa habari na kufanya mahojiano maalum kuhusu  sifa za mtu anayepewa Utemi katika ukoo wa Mtemi Milambo. 

Mzee huyo alisema, “Sisi kupewa Utemi inatokana na jinsi mtu alivyozaliwa au unabii unasemaje kuhusu mtu huyo.”

Alisema katika ukoo wa Milambo kabla ya Milambo hajazaliwa alianza Sibuga ambapo alipozaliwa ilishuka nyota moja, babu yake na Milambo aliyejulikana Kasele Muhofu aliongea akiwa bado tumboni mwa mama yake na ndio maana aliishi miaka 300, (1520-1820).

Mzee Solomoni alifafanua, “halafu alifuata shangazi Kibete alizaliwa akiwa malkia mwenye ziwa “titi moja” la mkono wa kushoto.”

“Mimi mwenyewe kabla ya kuzaliwa niliongea nikiwa tumboni mwa mama yangu na sikunyonya maziwa ya mama.” Aliongeza mzee huyo.

Mzee Solomoni alibainisha kuwa katika ukoo wa Milambo, mtu anayekabidhiwa mikoba ya Utemi ni lazima azaliwe kimaajabu au kuwe na unabii juu yake.

Alifafanua kuwa ikitokea akasimikwa Utemi mtu asiyetokana na maajabu au maelekezo maalumu hawezi kumaliza miezi miwili au mitano.

Siku hiyo ya Novemba 28, 2015, mzee Solomoni aliongoza jopo la wazee wa ukoo wa Milambo katika zoezi la kimila la kumsimika mbunge wa jimbo jipya la Ulyankulu John Peter Kadutu kuwa Mtemi.

Akizungumzia tukio hilo mzee huyo alisema kabla ya kumsimika mheshimiwa Kadutu nilioteshwa namna ya kumfanyia hivi na vila na kama nisingeoteshwa leo mvua isingenyesha.

Mzee Solomoni aliongeza “ndio maana mvua ilianza kunyesha kuanzia saa tatu asubuhi hadi muda ule tunafanya tambiko la kimila la kumsimika mheshimiwa Kadutu.”